#HABARI: Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Richard Abwao, amethibitisha kutokea kwa kifo cha Catherine Fito (21) Mkazi wa Umanda Kata ya Kalunde, Manispaa ya Tabora aliyejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu, ambapo chanzo cha kifo chake ikielezwa ni wivu wa kimapenzi.