#HABARI: Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza uteuzi mpya ndani ya Baraza Kivuli la Mawaziri, ambapo Wakili na Mwanaharakati maarufu nchini, Peter Madeleka, ametuliwa kuwa Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria.
Uteuzi huo umetangazwa leo, Juni 17, 2025, na Kiongozi wa Chama, Ndugu Dorothy Semu, ikiwa ni sehemu ya hatua ya chama hicho kuimarisha safu yake ya uongozi katika maeneo nyeti ya kisera na ushawishi wa kitaifa.