
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Fahrettin Altun ameilaani vikali Israel kwa hatua yake ya hivi majuzi inayowalenga wanahabari, na kuyataja mashambulizi hayo kuwa “ya kinyama” na “mashambulizi mabaya dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari.”
Katika taarifa yake siku ya Jumatatu, Altun alishutumu mgomo wa Israel kwenye televisheni ya taifa ya Iran, ambapo waandishi wa habari na raia waliripotiwa kuuawa.
“Shambulio la Israel dhidi ya Shirika rasmi la habari la IRNA, likiwalenga waandishi wa habari na raia, ni mauaji ya moja kwa moja. Kushambulia waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari ni unyama,” alisema katika ukurusa wa X.
Altun alitoa rambirambi zake kwa waandishi wa habari wa Iran waliouawa na kuishutumu serikali ya Israel kwa kupoteza uhalali wake kama taifa kutokana na ukiukaji wake wa mara kwa mara wa kanuni za kimataifa.
“Tunatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua dhidi ya uchokozi wa Israel na tabia ya kutojali ambayo inaifanya kanda hiyo kuwa na changamoto,” aliongeza.
Vitendo vya uvunjaji wa sheria
Katika taarifa tofauti, Altun pia alilaani polisi wa Israel kwa kuvuruga matangazo ya moja kwa moja ya mwandishi wa TRT Arabi Fehmi Shtewe na timu yake katika mji wa kaskazini wa Haifa.
Alisema vifaa vya timu hiyo vilichukuliwa na kwamba waandishi wa habari wa TRT Arabi na Alghad TV ya Misri walivurugwa.
“Serikali ya Israel, kwa bahati mbaya, inaendelea na vitendo vyake vya uvunjaji sheria vinavyoelekezwa dhidi ya waandishi wa habari wanaolilia ubinadamu wote kuhusu mauaji iliyofanya,” Altun alisema.
“Hili ndilo dhihirisho la hivi punde la ukichaa huu.”
Akiangazia kile alichokitaja kuwa kimya cha Magharibi, Altun alikosoa ukosefu wa mwitikio kutoka kwa taasisi za kimataifa ambazo mara nyingi hutetea maadili ya kidemokrasia.
“Tunawaachia maoni ya umma ya kimataifa kuhukumu ukimya wa nchi za Magharibi na taasisi zake za ‘kidemokrasia’ kuhusu ukiukaji huu, hasa ikiwa na wakati Israel ndiyo wahusika,” alisema.
Altun alihitimisha kwa kuthibitisha dhamira ya Ututuki ya kutetea uhuru wa vyombo vya habari na haki za wanataaluma wa vyombo vya habari:
“Tutaendelea kuwa wafuasi wenye bidii na watetezi wa uhuru wa kujieleza, uhuru wa kupokea habari, na haki za wanataaluma wa habari.”