#HABARI: Wanaotumia vyombo vya moto kuelekea Buguruni eneo la Riverside, barabara ya Mandela, wameendelea kukumbana na foleni inayochukua muda mrefu ambapo ITV imeshuhudia baadhi ya madereva wakiwa wameshuka kwenye magari yao wakiwa wamekata tamaa kwa kusubiri foleni hiyo ipungue.
Haijaweza kufahamika mara moja chanzo cha foleni hiyo ambapo jana Juni 09, 2025, njia hiyo pia ilikuwa na foleni kwa muda mrefu.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania.
#Follow @radioonetanzania