
Wizara ya afya ya Gaza imesema watu sita waliuwawa katika tukio hilo.
Kulingana na aliyeshuhudia, watu hao waliokuwa na silaha walionekana kushirikiana na jeshi la Israel baada ya kukimbilia katika maeneo ya kijeshi ya ya taifa hilo muda mfupi baada ya kurushiwa mawe na makundi ya watu waliokuwa wakishambuliwa.
Israel yazuia boti iliyobeba wanaharakati kuingia Gaza
Jeshi la Israel halikuweza kupatikana kutoa maoni yake juu ya madai hayo.
Wataalamu wameendelea kuonya kwamba mzingiro wa wanajeshi wa Israel katika maeneo ya wapalestina na kampani ya kijeshi dhidi ya kundi la Hamas kunaiweka Gaza katika hatari ya kukabiliwa na njaa.