Iran yaendelea kumiliki ujuzi wa ujenzi wa Mitambo ya Nyuklia

Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema kuwa Marekani imeshindwa kuzuia ujenzi wa mtambo wa nyuklia wa Karun katika jiji la Darkhovein, kusini magharibi mwa Iran, akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu inaendelea kufuatilia shughuli zake za nyuklia kwa amani licha ya njama za maadui.