Iran: Hatuchukui maagizo kutoka kwa yeyote kuhusu teknolojia ya nyuklia

Makamu wa Kwanza wa Rais, Mohammad Reza Aref amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko imara katika sera yake huru ya nyuklia na wala haishauriani au kuchukua maagizo kutoka kwa mtu yeyote yule.