Hujuma za waasi mashariki mwa Kongo zimeuwa watu 7,000 mwaka huu

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa watu zaidi ya elfu saba wameuawa mwaka huu wakati waasi wa kundi la M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wakiteka miji kadhaa katika eneo lenye utajiri wa madini mashariki mwa Kongo.