Hamas yaonya juu ya kuvunjika makubaliano ya kusitisha mapigano

Msemaji wa Brigedi za Izzuddin al Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiisamu ya Palestina HAMAS ametahadharisha kuhusu uwezekano wa kuvunjika makubaliano ya kusitisha vita kama utawala wa Kizayuni wa Israel utaendelea kufanya vitendo vinavyovunja vipengee vya makubaliano hayo.