HAMAS yakaribisha mpango wa Waarabu wa kuijenga upya Gaza

Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imekaribisha mpango wa kuikarabati na kuijenga upya Gaza, uliopitishwa katika mkutano wa dharura wa viongozi wa nchi za Kiarabu mjini Cairo, Misri. Mpango huo pia unakusudia kuzuia kuondolewa Wapalestinakatika eneo hilo lililo chini ya mzingiro.