HAMAS: Mateka 6 Waisrael wataachiwa leo mkabala wa Wapalestina 602 walioko kwenye jela za Israel

Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza majina sita ya mateka Waisrael, ambao wanatazamiwa kuachiliwa leo katika mwendelezo wa awamu ya kwanza ya makubaliano ya kusitisha mapigano na kubadilishana mateka na utawala wa Kizayuni wa Israel.