Hali ya wakimbizi Waislamu wa Rohingya waliofanyiwa ukatili mkubwa Myanmar bado ni mbaya

Hali mbaya ya Waislamu wa Rohingya, kabila la walio wachache kutoka Jimbo la Rakhine nchini Myanmar, inaendelea kuwa mbaya na kuliza walimwengu wenye hisia za kibinadamu huku kukiwa hakuna matumaini ya Waislamu hao kurejea kama walivyokuwa kabla ya kufanyiwa ukatili wa kutisha na mabudha na wanajeshi wa Myanmar.