Guterres ahudhuria futari ya Waislamu Warohingya wa Myanmar kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amefuturu na wakimbizi wa Rohingya walioko kwenye kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani, Cox Baazar nchini Bangladesh kuonyesha mshikamano na wakimbizi hao na wenyeji wanaowapa hifadhi.