Ghalibaf: Changamoto ya uhusiano wa kiuchumi wa Iran na Afrika ni usafiri

Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameyataja matatizo ya usafiri kuwa ni miongoni mwa changamoto kubwa katika kupanua uhusiano wa kiuchumi wa Iran na bara la Afrika akisema: Uwezo wa kimataifa kama wa kundi la BRICS na Shanghai ni fursa muhimu za kustawisha ushirikiano wa kiuchumi.