
KOCHA Mkuu wa Fountain Gate Princess, Camil Mirambo amesema wanahitaji kupata pointi tatu kwenye mechi ya leo dhidi ya Mashujaa Queens ili kuitafuta nafasi ya nne.
Timu hiyo iko nafasi ya nane kwenye msimamo na katika mechi 14, imeshinda nne, sare mbili na kupoteza nane ikikusanya pointi 14.
Ikipata ushindi kwenye mchezo huo, itasogea hadi nafasi ya sita na kufikisha pointi 17 na itaishusha Bunda yenye 15.