Fadlu ageuka mbogo Simba, acharukia mastaa

KOCHA wa Simba, Fadlu Davids amegeuka mbogo kwa kuwacharukia mastaa wa timu hiyo kutokana na matokeo ya mechi nne za viporo vya Ligi Kuu Bara, akiwakumbusha pia kazi iliyopo mbele yao katika fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane ya Morocco wikiendi hii ugenini.

Simba ilicheza na kushinda mechi hizo za viporo dhidi ya Mashujaa iliyoifunga mabao 2-1, ikailaza JKT Tanzania kwa bao 1-0 kisha kuicharaza Pamba Jiji 5-1 na juzi ikailaza KMC mabao 2-1 na kuvuna pointi 12 zilizopunguza pengo la pointi baina ya timu hiyo na vinara Yanga kutoka 13 hadi kuwa moja.

Lakini pamoja na ushindi huo wa mechi hizo nne mfululizo, kocha Fadlu ameonyesha kuchukizwa na kitendo cha ngome ya timu hiyo kuruhusu mabao katika mechi tatu, huku moja tu ndio wakipata clean sheet dhidi ya JKT Tanzania, jambo linalomtia presha wanapoenda kuikabili RS Berkane.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *