EU: Nchi wanachama wakubaliana juu ya mpango wa Brussels wa kuimarisha ulinzi wa Ulaya

Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya waliokutana katika mkutano wa kipekee mjini Brussels mnamo Machi 6, zimeidhinisha mpango kutoka Tume ya Ulaya kuimarisha ulinzi wao, ametangaza msemaji wa EU. Katika taarifa yao ya mwisho ya pamoja, viongozi wa Ulaya, isipokuwa Hungary, wamesisitiza uungaji mkono wao kwa Ukraine.

Imechapishwa:

Dakika 2

Matangazo ya kibiashara

Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, EU, wameidhinisha mapema Alhamisi jioni, Machi 6, mpango uliowasilishwa na Tume ya Ulaya “kuimarisha” ulinzi wa bara hilo. Nakal hiyo inalenga kuhamasisha, na kukusanya kwa muda mrefu, euro bilioni 800. Miongoni mwa chaguzi ni uwezekano wa nchi wanachama kuongeza kwa kiasi kikubwa matumizi yao ya kijeshi bila hii kuzingatiwa katika nakisi yao. “Maendeleo madhubuti kuelekea ulinzi mkali wa Ulaya”, hivi ndivyo mwanzilishi wa mkutano huu, Rais wa Baraza, Antonio Costa, alivyokaribisha ahadi iliyotolewa na nchi wanachama wa EU zimelazimishwa kwenye ukuta kufanya hivyo, wakiwa na wasiwasi juu ya hatua ya Marekani kutangaza kujiondoa.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema, huu ni mwanzo ukiwa ni hatua tu: “Kwa kuzingatia tishio na chochote kinachotokea nchini Ukraine, tunahitaji kuongeza uwezo wetu wa ulinzi na tunahitaji kujenga, katika miaka michache ijayo, uwezo wa ulinzi wa uhuru kwa nchi za Ulaya. Ninakaribisha chaguzi ambazo zimefanywa leo, lakini pia makubaliano mapana sana ambayo yameibuka kutoka kwa majadiliano yetu na ambayo, kwa macho yangu, yanaashiria ufahamu mkubwa kwa nchi za Ulaya na mwamko wa kina wa kimkakati. “

Rais wa Ufaransa pia alifichua kwamba alifuatwa na viongozi kadhaa huko Brussels kuhusu pendekezo lake la kupanua mwavuli wa nyuklia wa Ufaransa hadi Ulaya, anasema mwandishi wetu maalum huko Brussels, Anastasia Becchio. Wazo linalofaa kuzingatiwa, kulingana na Donald Tusk, Waziri Mkuu wa Poland. Wazo la kuvutia sana, kulingana na Rais wa Lithuania Gitanas Nauseda, lakini wazo pia lilielezewa mapema na viongozi wa Latvia na Czech. Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amesisitiza kuwa ni muhimu kutoacha ulinzi wa kijeshi wa Marekani.

Msaada kwa Ukraine umethibitishwa tena, lakini sio na Hungary

Viongozi wa Ulaya piame uungaji mkono wao kwa Ukraine katika taarifa kwamba Hungary haikujiunga. Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban yuko ni mshirika wa karibu wa Donald Trump na amedumisha uhusiano na Rais wa Urusi Vladimir Putin. Viongozi wa nchi hizo wamesema katika taarifa kwamba hakuwezi kuwa na mazungumzo juu ya Ukraine bila Ukraine – rejeleo la mazungumzo ya nchi mbili yaliyofunguliwa na Marekani na Urusi – na wameahidi kuendelea kutuma msaada kwa Kyiv, wakati Washington wiki hii ilizuia msaada wake wa kijeshi na kupeana taarifa za kiintelijia na Ukraine.