
Kinshasa imeamua kusitisha kwa muda wa miezi minne mauzo yake ya cobalt, ambayo hutumika haswa katika utengenezaji wa betri zinazoweza kuchajiwa. DRC inatoa robo tatu ya uzalishaji wa madini hayo duniani.
Imechapishwa:
Dakika 1
Matangazo ya kibiashara
Na mwanahabari wetu mjini Kinshasa, Coralie Pierret
Tangu mwaka 2016 cobalt imeuzwa chini sana katika soko la dunia: zaidi ya dola 20,000 kwa tani mwanzoni mwa mwaka ikilinganishwa na karibu dola 80,000 mwaka wa 2022. Hasara kubwa ya mapato kwa DRC. Kwa kuwa cobalt inajumuisha 15% hadi 20 ya mauzo yake ya nje.
Kwa hiyo DRC imeamua kusitisha mauzo ya nje kwa muda wa miezi minne, kupitia mamlaka yake ya udhibiti na udhibiti wa masoko ya kimkakati ya dutu za madini, ili kujaribu kuongeza bei ya madini hayo muhimu. Mwaka mmoja uliopita, Rais wa Kongo Félix Tshisekedi aliibua uwezekano wa kuanzisha viwango vya mauzo ya nje ya cobalt wakati wa mkutano wa baraza la mawaziri. “Tuwe a imani kwamba bei pia zitapanda ili kutoa malipo bora kwa wachimbaji wadogo,” anasema Eric Kalala, mkurugenzi wa ya Cobalt, kampuni tanzu ya kampuni ya umma ya Gécamines.
Lakini uamuzi huu utatosha? Hasa tangu uzalishaji wa kupindukia ambao unaelezea kushuka kwa bei kumeongezeka tangu moja ya makampuni makubwa ya sekta hiyo, kampuni ya China yaa Cmoc, kuzindua mgodi wa pili nchini DRC mwaka 2023.