DRC: Makundi ya Wazalendo yakabiliana Butembo

Mapigano makali yamezuka usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne (Machi 3 hadi 4) katikati mwa mji wa Butembo, mojawapo ya miji katika mko wa Kivu Kaskazini. Pande mbili za Wazalendo, wanamgambo wanaounga mkono serikali, walikabiliana magharibi mwa mji. Takriban wanamgambo tisa waliuawa kulingana na mashirika ya kiraia katika eneo hilo, sita kulingana na jeshi.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1

Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu mjini Kinshasa, Coralie Pierret

Mapigano hayo yalidumu kwa saa kadhaa kwenye vilima vya wilaya ya Kimemi katika mji wa Butembo. Kwanza alasiri ya Jumatatu tarehe 3 ili kuanza tena usiku wa Machi 3 kuamkia Jumanne Machi 4 kulingana na jeshi. Mapigano makali ambayo yalisababisha hofu katika mji huo wa kibiashara wa mkoa wa Kivu Kaskazini. Makundi mawili ya kambi moja yalirushiana risasi kwa sababu ambayo bado haijajulikana. Takriban wanamgambo tisa waliuawa, kulingana na mashirika ya kiraia. Hata hivyo, wote hao wanadai kuwa wanpiganaji wa Wazalendo, wanamgambo wanaoiunga mkono serikali.

“Ni kukosa heshima. “Ikiwa ni wazalendo, wote wanapaswa kuandamana nasi,” amejibu msemaji wa jeshi la Kongo katika eneo hilo, ambaye ametanaza kwamba wanamgambo sita ndio waliouawa katika video iliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii. Jeshi la Kongo kwa kweli linakabiliwa na umbali wa chini ya kilomita mia moja kusini na kundi la waasi la M23, linaloungwa mkono na Rwanda, ambalo katika wiki za hivi karibuni limepata mafanikio ya haraka katika mkoa huo, kuelekea Butembo.

Hatua ya kusonga mbele ambayo pia inaambatana na kuimarishwa kwa jeshi la Uganda katika eneo hilo, haswa katika eneo la Lubero. UPDF, ambayo hupiga doria mara kwa mara pamoja na vikosi vya Kongo, iliingia DRC mnamo mwezi wa Novemba 2021, awali ili kuangamiza ADF, kundi lililoanzishwa na waasi wa Uganda, wanaoshirikiana na Islamic State.