Christopher Hedges: Nasikitishwa na tabia ya kuwataja Waislamu kuwa ni mashetani

Mwandishi wa habari wa Marekani, Christopher Hedges, amesema anasikitishwa na jinsi Waislamu wanavyodhihirishwa katika nchi za Magharibi katika sura ya mashetani akisisitiza kwamba utamaduni wa Kiislamu ni tofauti kabisa na sura potovu inayowasilishwa.