Changamoto zinazoikabili Ulaya mbele ya Sera za Trump: Wasiwasi na wahka

Wakati Donald Trump akianza muhula wake wa pili kama Rais wa Marekani, nchi za Ulaya zimeingiwa na wasiwasi na wahka mkubwa kuhusu sera zake. Sasa, maafisa wa nchi za Ulaya wanatafuta njia za kushughulikia changamoto zinazojitokeza baina pande hizo mbili, kuanzia kwenye vitisho vya kibiashara hadi masuala ya usalama.