Chamou atibua hesabu Simba

KAMA utani hivi, beki wa kati Simba, Chamou Karaboue amebadili uamuzi wa mabosi wa klabu hiyo kutokana na kiwango chake, huku kocha wa kikosi hicho, Fadlu Davids akisema amefanikiwa kuwapa changamoto Che Malone Fondoh na Abdulrazack Hamza.

Muivory Coast huyo ambaye alitua Simba msimu huu, alikuwa hana mwanzo mzuri kutokana na Che Malone na Hamza kuwa na uwezo mkubwa uliomshawishi kocha Fadlu muda mwingi kuwatumia.

Mwanaspoti linafahamu kuwa kabla ya Che Malone kuumia miezi ya karibuni, Simba ilikuwa inafikiria kusajili beki wa kati mwigine wa kigeni na kuachana na Muivory Coast huyo, lakini kiwango alichoonyesha Chamou kimebadilisha mtazamo wa benchi la ufundi na hata mabosi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *