Canada: Wanasiasa kufanya mjadala chini ya wiki mbili kabla ya uchaguzi wa wabunge

Viongozi wa vyama vikuu vya siasa nchini Canada watakutana siku leo Jumatano jioni kwa mdahalo kwa lugha ya Kifaransa huko Montreal, ambapo mkuu wa chama cha kiliberal Mark Carney atakuwa chini ya uangalizi wa kipekee katika hali hii  ya kampeni ya uchaguzi inayotawaliwa na mivutano na Marekani ya Donald Trump.

Imechapishwa:

Dakika 2

Matangazo ya kibiashara

Waziri Mkuu mpya wa Canada, ambaye alichukua nafasi ya Justin Trudeau katikati ya mwezi Machi na kuitisha uchaguzi wa mapema katika mchakato huo, anatarajiwa kuleta mabadiliko katika umilisi wake wa Kifaransa na ulinzi wa jimbo linalozungumza Kifaransa la Quebec, masuala muhimu katika nchi hii yenye lugha mbili.

Kulingana na tafiti, baadhi ya 40% ya wapiga kura katika nchi hii ya G7 yenye watu milioni 41 bado hawajafanya chaguo lao, chini ya wiki mbili kabla ya uchaguzi uliopangwa kufanyika Aprili 28.

“Tofauti na kawaida, nasubiri mjadala utoe maoni,” Carole Potvin ameliambia shirika la habari la AFP. “Sijawahi kupigia kura chama cha kiliberali, lakini leo natafakari kwa hilo. Vitisho vya Donald Trump vimebadilisha kila kitu.”

kurejea kwa Donald Trump ikulu ya White House, ambaye ametoza ushuru wa forodha kwa jirani yake wa kaskazini, ambaye ana ndoto ya kuifanya kuwa jimbo la 51 la Marekani, kumebadilisha kadi za siasa za Canada.

Waziri mpya wa Canada, mwenye umri wa miaka 70, ambaye anatoka mkoa wa Montreal, anaeleza kwamba kwa hivyo hatazingatia kiwango cha Kifaransa kwa wagombea, lakini anasema anataka kusikia maneno makali kuhusu kutetea jimbo hilo linalozungumza Kifaransa.

Hotuba hiyo hiyo kutoka kwa Alexandre Tittley. Kwa mbunge huyu wa Quebec mwenye umri wa miaka 50, anasema “tuna hali ya kuchukiza duniani kwa sababu ya Trump, na tunachotafuta zaidi ya yote ni kiongozi mwenye msimamo.”

Baada ya kubadili kabisa mwelekeo huo katika wiki za hivi majuzi, Wanaliberali (katikati) wanatawala nia ya kupiga kura (44%) mbele ya Conservatives (kulia) iliyopewa 38%. Nyuma yao kinakuja chama cha New Democratic Party (NDP, kushoto) kwa 8%, kisha Bloc Québécois, chama kinachotetea kujitengwa kutoka Quebec, kwa 6%.

– Mjadala umechelewa –

Mbali na lugha mbili, mjadala huu wa wanaume wote utafuatiwa na mdahalo wa pili, kwa Kiingereza, siku yaAlhamisi. Utajikita kwenye masuala nyeti zaidi ya kampeni: ushuru, vitisho vya Donald Trump, shida ya makazi, mfumuko wa bei, na mustakabali wa nishati nchini.

Siku ya Jumanne, dakika za mwisho, mdahalo ulisogezwa mbele kwa saa mbili, hivyo sasa utafanyika Jumatano saa 12:00 jioni saa za Canada (saa 6 usiku saa za Ufaransa).

Kwa upande wa wapiga kura wanasema mjadala utakuwa fursa ya kulinganisha moja kwa moja maono ya Mark Carney, Pierre Poilievre, Jagmeet Singh wa NDP, Yves-François Blanchet wa Bloc Québécois na Jonathan Pedneault (Green Party).

Kifaransa chake kiko vizuri kuliko kile cha Pierre Poilievre, “ikiwa atafanya vizuri bila kufanya makosa yoyote, itakuwa ushindi,” anasema Daniel Béland, profesa wa sayansi ya siasa katika Chuo Kikuu cha McGill.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *