Amnesty yataka kuchunguzwa jinai za kivita za Israel nchini Lebanon

Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa mwito wa kufanyika uchunguzi huru juu ya mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya vituo vya matibabu, magari ya dharura na wafanyakazi wa afya nchini Lebanon, na kutaja hujuma hizo kama uhalifu wa kivita.