Al-Azhar yawataka Waarabu na Waislamu kupinga kufukuzwa Wapalestina Gaza

Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al-Azhar nchini Misri kimesisitiza kwa mara nyingine tena juu ya kupinga mpango wa kufukuzwa Wapalestina wa Gaza kutoka katika ardhi yao na kuwataka Waarabu na Waislamu kujitokeza na kupinga mpango huo.