Abu Sharif: Wananchi wa Gaza wamezuia ushindi wa utawala wa Israel

Mwakilishi wa harakati ya Jihad Islami ya Palestina mjini Tehran amesema: Licha ya uchache wa suhula waliokuwa nao, wananchi wa Gaza waliweza kuendeleza mapambano yao ya ukombozi na kuzuia kusonga mbele utawala wa Kizayuni kutokana na uungaji mkono na msaada mkubwa wa Mhimili wa Muqawama unaojumuisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Lebanon, Iraq na Yemen.