Israeli inasema inaanzisha mashambulizi mapya kufuatia jibu la Iran

Jeshi la Israel limesema siku ya Jumamosi kwamba lina udhibiti wa anga “magharibi yote ya Iran, hadi Tehran,” likidai kuwa limeshambulia ndege 70 za kivita usiku kucha. “Tumeunda uhuru wa kuchukua hatua za anga katika eneo lote la magharibi mwa Iran, hadi Tehran,” amesema Brigedia Jenerali Effie Defrin, msemaji wa jeshi la Israeli, katika mkutano na waandishi wa habari.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ndege za Israeli sasa zinaruka “kwa uhuru kamili” juu ya mji mkuu wa Iran, amebainisha, na “Tehran haiko salama tena.” “Usiku mmoja, Jeshi la Wanahewa lilifanya mashambulizi yaliyohusisha zaidi ya ndege 70 za kivita dhidi ya malengo ya kijeshi huko Tehran […] eneo lenye kina kirefu zaidi katika eneo la Iran ambapo tumefanya operesheni hadi sasa,” jenerali huyo aliongeza.

Jeshi la Israeli lilitangaza saa sita mchana siku ya Jumamosi kuwa “kwa sasa” limeanzisha mashambulizi dhidi ya maeneo kadhaa nchini Iran, kufuatia mashambulizi ya makombora ya Iran kujibu mashambulizi makubwa ya Israeli siku moja kabla. “Kwa sasa tunaanzisha mashambulizi dhidi ya maeneo kadhaa nchini Iran,” amesema msemaji wa jeshi la Israeli Brigedia Jenerali Effie Defrin katika taarifa.

Iran inasema mazungumzo na Marekani “hayana maana” katika hatua hii

Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Jumamosi kwamba “haina maana” kwa Iran kufanya mazungumzo yaliyopangwa na Marekani kuhusu mpango wake wa nyuklia siku ya Jumapili, kutokana na mashambulizi ya Israeli dhidi ya nchi hiyo. “Ni dhahiri kwamba katika mazingira kama haya, na maadamu hujuma za utawala wa Kizayuni dhidi ya taifa la Iran zinaendelea, hakutakuwa na maana ya kufanya mazungumzo na upande ambao ni muungaji mkono na mshirika mkubwa wa mvamizi,” msemaji wa wizara hiyo Esmaeil Baqaei amesema katika taarifa yake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *