Marekani: Seneta wa Democrat afukuzwa kwenye mkutano rasmi na wanahabari na kufungwa pingu

Nchini Marekani, seneta kutoka chama cha Democratic ameondolewa kwa nguvu kwenye mkutano Waziri wa Usalama wa Ndani aliokuwa akifanya na waandishi wa habari huko Los Angeles. Tukio hili linaonyesha zaidi mvutano kati ya Democrats na Republicans kuhusu kukamatwa na kufukuzwa kwa wahamiaji wasio na vibali na maandamano huko California.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu nchini Marekani, Loubna Anaki

Picha za tukio hilo zimesambaa mara moja kwenye vyombo vya habari vya Marekani, na kusababisha mzozo kati ya Republicans na Democrats. Katika video hiyo, wakati Kristi Noem, Waziri wa Usalama wa Ndani, akiongea kutetea kukamatwa kwa watu wengi wa wahamiaji wasio na vibali, Seneta Alex Padilla anaonekana kumkatisha: “Mimi ni Seneta Alex Padilla, na nina maswali kwa waziri,” anasema, kabla ya kusukumwa nje mara moja na maafisa wa usalama na kufungwa pingu na kuondolewa.

Akamatwa kwa kumshuku kuwa ni msumbufu? 

Baadaye kidogo, seneta wa California amezungumza na waandishi wa habari: “Ikiwa hivi ndivyo serikali inavyojibu maswali ya seneta, tunaweza kufikiria tu jinsi wanavyowatendea wafanyikazi wasio na vibali kwenye mashamba, jikoni, kote Los Angeles na kote California.”

Kristi Noem ameeleza kuwa maafisa walifanya hivi wakidhani kwamba alikuwa msumbufu. Anabaini kwamba seneta huyo alifanya mambo “yasiyofaa.” Ameongeza, hata hivyo, kwamba alizungumza naye kwa dakika chache baada ya mkutano na waandishi wa habari. Wademocrats, kwa upande wao, wanachukulia kile alichofanyiwa mwenzao kuwa ni kitendo cha “kukasirisha.” Wapo wanaotaka Waziri wa Usalama wa Taifa ajiuzulu.

“Tabia kama ya mtoto”

Msemaji wa Ikulu ya White House, Karoline Leavitt amesema kwenye mtandao wa kijamii wa X kwamba “Seneta Padilla anapaswa kuaibishwa na tabia yake ya kitoto.” Katika Bunge la Congress, shirika la habari la AFP linaripoti, takriban wabunge kumi wenye asili ya Uhispania walitembelea ofisi za Spika wa Bunge Mike Johnson, kutoka chama cha Republican, kumwomba amtetee mwenzao na “taasisi ya Congress, dhidi ya utawala unaopinga demokrasia.” “Kuna kampeni ya vitisho kujaribu kunyamazisha upinzani,” Mwakilishi afisa aliyechaguliwa kutoka chama cha Democratic Adriano Espaillat amesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *