Huku maandamano yakienea kote Marekani, amri ya kutotoka nje wakati wa usiku imekuwa ikiwekwa katika jiji la pili kwa ukubwa huku mamlaka zikikabiliana na uharibifu na uporaji ambao uliharibu vizuizi vichache vya jiji.Polisi yakamata idadi kubwa ya watu Los Angeles
Trump alisema katika mtandao wa Truth Social kwamba walinzi wa kitaifa kwa kushirikiana na wanajeshi wamewasaidia polisi wa LA kufanya kazi yao kwa ufanisi, akiongeza kuwa bila ya wanajeshi jiji hilo lingegeuka kuwa sehemu ya uhalifu ambao haujashuhudiwa katika miaka ya karibuni.
Maandamano mengi ya amani yalianza wiki iliyopita kutokana na kuongezeka kwa juhudi za kuwakamata wahamiaji nchini humo kinyume cha sheria, lakini pia kulikuwa na vurugu, ikiwa ni pamoja na uchomaji wa teksi zinazojiendesha na kuwarushia mawe polisi.
Trump aliamuru kutumwa wanajeshi elfu kadhaa wa jeshi la walinzi wa kitaifa na wanamaji 700 huku gavana wa CaliforniaGavin Newsom, akipinga hatua hiyo. Trump alieleza kuwa gavana huyo alikuwa amepoteza udhibiti wa hali akimtaka ashukuru badala ya kutetea makosa yako na kukosa ufanisi.
Huko Spokane, kaskazini-magharibi mwa jimbo la Washington, amri nyingine ya kutotoka nje usiku ilitangazwa baada ya polisi kuwakamata zaidi ya waandamanaji 30 na kurusha mipira ya pilipili ili kutawanya umati wa watu.
Huko Seattle, mji mkubwa wa jimbo la Washington, polisi waliwakamata watu wanane baada ya dampo kuchomwa moto na vilipuzi kurushwa. Watu watatu walikamatwa huko Tucson, Arizona, kufuatia makabiliano na polisi huku maandamano pia yakifanyika Las Vegas, Dallas, Austin, San Antonio, Milwaukee, Chicago, Atlanta, na Boston, kulingana na CNN.