Ujerumani yaahidi msaada zaidi kwa Ukraine

Akizungumza na waandishi wa habari Pistorius amesema, Madhumuni ya ziara hiyo ni kuonyesha kwamba serikali mpya ya Ujerumani, inaendelea kusimama na Ukraine katika hali ya sasa, ambayo bado ni tete. Pistorius almeongeza kusema kwamba atazungumzia msaada zaidi wa silaha kutoka Ujerumani na mataifa ya Ulaya.

Kabla ya kuondoka Ujerumani Pistorius alisema wanafanya kila wawezalo kuhakikisha Ukraine inajilinda na kuimarisha nafasi yake katika mazungumzo yoyote ya baadaye na Urusi.

Ujerumani ni mfadhili wa pili kwa ukubwa wa kijeshi kwa Ukraine baada ya Marekani, ambayo msaada wake kwa Kyiv umeanza kutiliwa shaka, na hivyo kuiweka Ulaya chini ya shinikizo la kuongeza msaada wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *