
Wakati Rais waKenya William Ruto akipuuzilia mbali matukio yaliyotolewa awali na vyombo vya usalaam kueleza kifo cha kijana huyo akiwa kizuizini, mkuu wa polisi ameomba msamaha kwa niaba ya idara hiyo kwa kushikilia kuwa Albert Ojwang alifariki baada ya kugonja kichwa chake katika ukuta wa chuma alikokuwa aanazuiliwa.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Utata unaendelea kutanda nchini Kenya kufuatia kifo cha Albert Ojwang, mwanamume mwenye umri wa miaka 31 aliyekamatwa Jumamosi, Juni 7, na ambaye alifariki usiku uliofuata akiwa kizuizini. Wakati matokeo ya uchunguzi wa maiti uliofanyika Jumanne, Juni 10, kwenye mwili wa mwathiriwa yalipingana na toleo la awali la polisi kwamba aligonga kichwa chake kwenye ukuta wa chumba alikokuwa anazuiliwa—badala yake, yamerejelea majeraha “yaliyosababishwa na kitu alichopigwa kutoka nje,” yakibainisha kwamba alikuwa mlengwa wa shambuli – watu wameendelea kutoa hisia zao kote nchini.
Katika kujaribu kupata majibu ya maswali mengi ambayo bado yanahusu mazingira ya kifo cha Albert Ojwang, maseneta wa Kenya waliwaita maafisa kadhaa wakuu wa usalama siku ya Jumatano, Juni 11, akiwemo mkuu wa polisi, Douglas Kanja, anaripoti mwanahabari wetu mjini Nairobi, Albane Thirouard. Baada ya kuhojiwa kwa nguvu, mwishowe alikubali makosa, akieleza kuwa “sio kweli kwamba Albert Ojwang aligonga kichwa chake ukutani.”
“Naomba radhi kwa niaba ya polisi kwa taarifa hii,” amekiri kabla ya kuahidi kuchukuliwa hatua za kinidhamu mara baada ya matokeo ya uchunguzi kujulikana. Katika suala hili, IPOA, jeshi la polisi, limehakikisha kuwa ripoti yake itakuwa tayari ndani ya siku kumi. Hata hivyo, naibu mkuu wa IPOA amesikitishwa na kukosekana kwa picha za CCTV kutoka usiku husika, ambao alisema alikuwa daktari.
“Tukio la kusikitisha, lililofanywa na polisi, la kuvunja moyo na lisilokubalika”
Kulingana na Gazeti la Kenya Today, maseneta hao pia wametaka kukamatwa mara moja kwa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Eliud Kipkoech Lagat—aliyehusika na kukamatwa kwa Albert Ojwang—na kutaka ashtakiwe kwa kuamuru mauaji ya kijana huyo.
Siku ya Jumatano, toleo la matukio yaliyotolewa hapo awali na vikosi vya usalama pia limetupiliwa mbali na taarifa kutoka kwa Mkuu wa Nchi, ambapo William Ruto ameeleza kuwa “tukio la kusikitisha, lililofanywa na polisi, […] la kuvunja moyo na lisilokubalika.”
Hatimaye, wanaharakati kadhaa wa haki za binadamu na mashirika yasiyo ya kiserikali wametaka uchunguzi ufanyike kwa uwazi kabisa, wakihofia kuwa maafisa wa ngazi za chini wanaweza kuteuliwa kuhusishwa katika mauaji haya wakati waliagizwa na wakuu zao. Kwa kuzingatia hayo, Gazeti la kila siku la Kenya The Standard lilichapisha majina yaliyotolewa na mamlaka ya maafisa watano wa polisi waliokuwepo wakati wa kitendo hicho kiovu.
Hasira inaendelea kushika kasi mtandaoni
Kuitwa kwa maafisa wa polisi na maseneta pia kulifafanua mazingira ambayo Albert Ojwang alikamatwa. Ijapokuwa ilijulikana kuwa kukamatwa kwake kulitokana na malalamiko kutoka kwa nambari mbili katika vikosi vya usalama, kikao chao kiliangazia ukweli kwamba Eliud Lagat alikuwa amewasilisha baada ya Albert Ojwang kuchapisha jumbe kadhaa ambazo hazikujulikana zikimshtumu kwa ufisadi-ikiwa ni pamoja na kuwaweka maafisa chini ya udhibiti wake katika nyadhifa zinazodhibiti fedha.
Vyovyote vile, wito wa kujiuzulu kwa Eliud Lagat umeendelea kuongezeka katika siku za hivi karibuni, huku kesi hiyo ikiendelea kuzua hasira kubwa mitandaoni, mwaka mmoja tu baada ya ukandamizaji wa umwagaji damu kwenye maandamano ya Juni 2024, ambapo vikosi vya usalama vinashutumiwa na makundi kadhaa ya haki za binadamu kwa kuua watu wasiopungua 60 na kuwateka nyara makumi ya wengine.