
Mpango huo uliotiwa saini wiki iliyopita, unawazuwia raia kutoka Afghanistan, Myanmar, Chad, Jamhuri ya Kidemokrai ya Kongo, Equatorial Guinea, Eritrea, Haiti, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen kuingia nchini Marekani.
Maelfu ya waandamanaji wajitokeza kupinga sera za Trump Marekani
Pia unaweka masharti ya kusafiri kwa raia wa Burundi, Cuba, Laos, Sierra Leone, Togo, Turkmenistan na Venezuela ambao wapo nje ya Marekani na wasiokuwa na vibali halali.
Mpango huo hata hivyo haubatilishi visa zilizokuwa tayari zimetolewa kwa watu wa mataifa yaliyotajwa kabla ya mpango wenyewe kupitishwa.