Rwanda yajiondoa katika Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati

Rwanda imetangaza kujiondoa katika Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati (ECCAS) kufuatia mkutano wa 26 wa shirika hilo siku ya Jumamosi, Juni 7, mjini Malabo. Kigali imeshutumu kushindwa kwake kushika urais wa zamu na kueleza masikitiko yake juu ya “kutumiwa kwa ECCAS na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa kuungwa mkono na baadhi ya nchi wanachama.”

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati (ECCAS) umeongeza muda wa urais wa Rais wa Equatorial Guinea kwa mwaka mwingine siku ya Jumamosi, huku kukiwa na mvutano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda.

Uamuzi huo ulichukuliwa mwishoni mwa kikao cha 26 cha kawaida cha ECCAS, kilichofanyika Jumamosi huko Malabo, Equatorial Guinea, mbele ya wakuu saba wa nchi kumi na moja wanachama. “Mkutano umeahirisha mpito wa urais wa zamu wa Jumuiya ambao Jamhuri ya Rwanda ndio imekuwa imefikiwa kushikilia na kwa hivyo kuamua Bw. [Teodoro] Obiang Nguema Mbasogo, raia wa sasa wa ECCAS kuendelea kushikilia urais wa zamau wa jumuiya hiyo kwa muda wa ziada wa mwaka mmoja,” imesema taarifa ya mwisho ya mkutano huo.

Kulingana na kamishna aliyenukuliwa na shirika la habari la AFP, wawakilishi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waliripotiwa kubishana kwamba hawataweza kuhudhuria shughuli za Jumuiya ikiwa wangepokelewa na Rwanda. Rwanda imeshutumu kuwekewa mashaka kwa haki zake inazopewa na sheria zinazounda Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati (ECCAS) na kushtumu “kushindwa kwa jumuiya hiyo kutekeleza sheria zake.”

Hata hivyo, wakati wa mkutano huu huko Malabo, ECCAS imeamua kuzindua eneo la biashara huria la Jumuiya mnamo Agosti 30, 2025.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *