Watu kadhaa wauawa katika mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine

Mashambulizi ya Urusi katika miji ya Kharkiv na Kherson nchini Ukraine yamesababisha vifo vya watu watano na takriban 17 kujeruhiwa usiku wa Ijumaa Juni 6 kuamkia Jumamosi Juni 7, mamlaka katika miji hiyo ya Ukraine zimetangaza.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Watu watatu wameuawa katika shambulio kubwa huko Kharkiv, ametangaza Igor Terekhov, meya wa jiji hilo la pili kwa ukubwa nchini Ukraine, na wawili waliuawa huko Kherson, kulingana na gavana wa mkoa wa Kherso, Oleksandr Prokudin.

Mvua ya mawe ya mabomu imenyesha nchini Ukraine. Mashambulizi ya Urusi katika miji ya Kharkiv na Kherson yameua watu watano na kujeruhi zaidi ya 20 usiku kucha kuanzia Ijumaa hadi Jumamosi, Juni 7, baada ya Moscow kuahidi “jibu” kwa uharibifu wa sehemu ya meli zake za anga siku ya Jumapili.

Vifo vitatu na takriban majeruhi 17 vimeripotiwa katika mji wa Kharkiv, mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine, ambao umekumwa na “shambulio lenye nguvu zaidi tangu kuanza kwa vita” mnamo mwezi 2022, kulingana na meya wa mji huo, Igor Terekhov.

Kwa jumla, “angalau milipuko 40” imesikika ndani ya muda mfupi katika jiji hili lenye wakaaji milioni 1.4 lililoko chini ya kilomita 50 kutoka mpaka wa Urusi kaskazini-mashariki mwa nchi.

“Adui anapiga kwa wakati mmoja na makombora, ndege zisizo na rubani za Shahed, na mabomu ya angani,” meya wa Kharkiv ameeleza, akiongeza kuwa angalau drone 48 za Shahed, makombora mawili, na mabomu manne yametumiwa.

Watu wawili wameuawa katika wilaya ya Kyivsky na mwingine katika wilaya ya Osnovyansky, na karibu ishirini wamejeruhiwa, aliripoti.

Wanandoa wa umri wa miaka hamsini pia walikufa katika shambulio lililopiga majengo mawili huko Kherson, kusini, kulingana na gavana wa Kherson, Oleksandr Prokudin. Watu wawili wamejeruhiwa, kama vile wengine wawili katika mkoa wa Dnipropetrovsk (mashariki).

Urusi ilifanya moja ya mashambulizi yake makubwa tangu kuanza kwa vita usiku wa Alhamisi kuamkia Ijumaa, ikiwa na ndege zisizo na rubani 407 na makombora 45, kulingana na jeshi la Ukraine.

Idadi ya waliofariki kutokana na shambulizi hili iliongezeka hadi angalau watano siku ya Jumamosi na kupatikana kwa mwili wa mwanamke kwenye vifusi huko Lutsk, karibu na mpaka wa Poland.

Ukatili wa Moscow

Moscow ilizungumza siku ya Ijumaa kuhusu “jibu” baada ya mashambulizi ya Ukraine ambayo yalilenga viwanja kadhaa vya ndege vya Urusi vilivyo mbali na mstari wa mbele siku ya Jumapili, na kuharibu ndege kadhaa za kivita.

Mashambulio haya yanakuja wakati mazungumzo ya amani yamekwama kufuatia duru ya pili ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Urusi na Ukraine mjini Istanbul siku ya Jumatatu, ambayo yalishindwa kufikia usitishaji mapigano.

“Kwetu sisi, hili ni suala linalowezekana, moja ya masilahi yetu ya kitaifa, usalama wetu, maisha yetu ya baadaye na ya watoto wetu,” msemaji wa rais wa Urusi Dmitry Peskov amesema.

Shambulio hili lilisababisha kufungwa kwa uwanja wa ndege mkuu wa Moscow, Sheremetyevo, kulingana na mamlaka ya anga.

Majeshi ya Urusi, ambayo yanachukua takriban 20% ya eneo la Ukraine yamekuwa yakishambulia miji ya Ukraine karibu kila siku tangu mwaka. Kujibu, Ukraine pia hufanya mashambulizi ya anga nchini Urusi karibu kila siku.

Huko Kharkiv, jiji ambalo lina watu wengi wanaozungumza Kirusi, watu 18, wakiwemo watoto wanne, walijeruhiwa katika mashambulizi ya Urusi siku ya Alhamisi.

Jeshi la Ukraine lilitangaza Ijumaa kuwa “limefanikiwa” kushambulia kwa mabomu vituo vingine viwili vya anga nchini Urusi usiku, katika mikoa ya Saratov na Ryazan (katikati mwa Urusi), wakidai kushambulia vituo vya mafuta.

Urusi na Ukraine watabadilishana wafungwa 500 wa vita kutoka kila upande mwishoni mwa juma hili, kufuatia mabadilishano ya hapo awali ya watu 1,000 kila upande mwezi Mei. Pia walikubali kukabidhi miili ya maelfu ya wanajeshi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *