
Mswaada wa amani umewasilishwa kwa serikali ya Jamhuri wa Kidemokrasia ya Kongo na kwa waasi wa M23 baada ya kufanyika mazungumzo nchini Qatar. Wapatanishi wa Qatar wamewasilisha mswada huo wa amani kwa pande zote mbili kwa ajili ya mashauriano kabla ya kurejea na kuendelea na mazungumzo.
Mazungumzo yaliyofanyika mjini Doha hivi karibuni yalizingatia masuala ya msingi yaliyosababisha mgogoro.
Wapiganaji wa M23 ambao kwa mujibu wa wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamekuwa wanaungwa mkono na Rwanda wamesonga mbele kwa haraka mashariki mwa Kongo tangu mwezi wa Januari. Wameiteka miji muhimu na maeneo makubwa katika mapigano yaliyosababisha vifo vya maelfu ya watu.
Qatar imeshirikiana na Marekani katika juhudi za kuutatua mgogoro wa nchini Kongo.