
Amesema kiongozi huyo wa Urusi ameapa kulipiza kisasi baada ya Kyiv kushambulia viwanja vyake vya ndege za washambuliaji wa Urusi.
Trump amesema kupitia mtandao wake wa kijamii ya Truth kwamba ingawa yalikuwa mazungumzo mazuri, lakini bado hayafungui njia ya kupatikana amani ya haraka. Lakini Kremlin ilisema yalikuwa yenye tija.
Mazungumzo yao yamefanyika siku tatu baada ya Ukraine kushambulia kambi za kijeshi za Urusi, ikisema imeharibu ndege kadhaa za thamani ya mabilioni ya dola.