Chad: Watu 41 wafariki katika makabiliano kusini mwa nchi

Nchini Chad, dazeni kadhaa za watu wamefariki katika “makabiliano makali” katika kijiji cha Mandakao, katika jimbo la Logone Occidental, karibu na mpaka wa Cameroon. Kulingana na vyanzo rasmi, idadi ya waliofariki imefikia 41 na majeruhi kadhaa.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu huko Ndjamena, Nadia Ben Mahfoudh

Kijiji cha Mandakao kilishambuliwa siku ya Jumatano, Mei 14. Kulingana na chanzo cha mahakama, kambi mbili za watu wa kuhamahama na takriban vibanda 80 vilichomwa moto. “Wakazi waliuawa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto,” kulingana na chanzo kimoja. Watu kadhaa waliojeruhiwa walisafirishwa hadi hospitali ya wilaya ya Beinamar, takriban kilomita 80 kutoka Moundou. Baadhi yao walifariki kutokana na majeraha yao.

“Mauaji mabaya  kabisa”

Watu kadhaa waliopo Mandakao wanaeleza kuwa mzozo baina ya jamii ndio chanzo cha makabiliano haya. “Mgogoro wa aina hii upo,” kimesema chanzo cha mahakama, “lakini hali ni mbaya zaidi kuliko kawaida.” Kabla ya kuongeza kwamba “mauaji hayo yalikuwa mabaya sana. Mauaji hayo yamesababisha maombolezo katika kijiji kizima.”

Utulivu warejea

Sababu haswa bado hazijafahamika, uchunguzi umefunguliwa ili kutoa mwanga juu ya suala hilo. Vikosi vya ulinzi na usalama vya Chad, vilivyotumwa haraka kwenye eneo la tukio, tayari vimewakamata watu 82 kama sehemu ya uchunguzi unaoendelea. Siku ya Alhamisi, Waziri wa Usalama na Waziri wa Tawala za Mikoa walizuru kijiji hicho na hali ya utulivu imerejea.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *