Putin hayupo kwenye orodha ya mazungumzo kuhusu Ukraine nchini Uturuki

Ukraine na Urusi kwa mara ya kwanza zinatarajiwa kuwa na mazungumzo ya ana kwa ana baada ya zaidi ya miaka 3 tangu mataifa hayo yaingie vitani, huku rais Vladmir Putin akiwa hayuko kwenye orodha ya ujumbe utakaosafiri kwenda Uturuki.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1

Matangazo ya kibiashara

Awali rais wa Ukraine, Volodymry Zelensky alimtaka rais Putin kukutana nae ana kwa ana mjini Instanbul, kuonesha kweli ana nia ya kupata suluhu ya mzozo unaoendelea, hata hivyo Urusi imeamua kutaja timu ya ujumbe wa kawaida kushiriki mazungumzo hayo.

Wachambuzi wa mambo wanasema kutokuwepo kwa rais Putin ni pigo jingine katika juhudi za kusaka suluhu ya vita kati ya nchi yake na Ukraine.

Rais wa Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesisitiza kwamba yuko tayari kwa mazungumzo hayo kuelekea kupatikana kwa amani.
Rais wa Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesisitiza kwamba yuko tayari kwa mazungumzo hayo kuelekea kupatikana kwa amani. © Evgeniy Maloletka / AP

Wiki iliyopita rais Putin alipendekeza Mei 15 yafanyike mazungumzo ya amani ya moja kwa moja kati yake na Ukraine, kauli iliyoonekana kama ishara chanya, ingawa viongozi kadhaa wa Ulaya walihoji utashi wa Moscow.

Vyanzo vya kidiplomasia vilivyo karibu na mchakato ulioanzishwa na Marekani, vinasema kutokuwepo kwa maofisa wa juu toka Moscow na Washington, ni ishara ya wazi kuwa hakuna hatua itakayopigwa kuelekea usitishwaji wa kudumu wa mapigano.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *