Fadlu avujisha za Orlando, Tshabalala naye kumekucha

KOCHA Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amefichua ujumbe alioupokea kutoka kwa mmoja wa maofisa wa juu wa Orlando Pirates ya Afrika Kusini baada ya kufuzu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Timu hiyo imefuzu fainali mara ya kwanza tangu michuano hiyo ilipoasisiwa 2004 kwa kuunganishwa Kombe la CAF na la Washindi, na imepangwa kukutana na RS Berkane kati Mei 17 na 25 ambapo mshindi wa jumla atabeba taji hilo lililotemwa na Zamalek ya Misri.

Simba itaanzia ugenini kabla ya kumalizia nyumbani Mei 25 ikiwa na kazi ya kulipa kisasi dhidi ya timu hiyo ya Morocco iliyowahi kukutana nayo katika makundi ya michuano hiyo msimu wa 2021-2022 na kila moja kushinda mechi ya nyumbani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *