
Rais Samia Suluhu Hassan, ametoa ahadi ya Sh30 milioni kwa nyota wa Simba kwenye kila bao litakalofungwa kwenye mechi ya fainali.
Simba inatarajia kucheza fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane baada ya kutinga hatua hiyo kwa kuifunga Stellenbosch ya Afrika Kusini kwa ushindi wa bao 1-0.
Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Rais Samia anawapongeza Simba kwa kutinga hatua ya fainali na anawatakia kila la kheri kwenye mechi mbili za fainali zilizo mbele yao kwa kutoa ahadi ya kununua kila bao watakalofunga kwa Sh30 milioni.