Mjadala umeanza kuhusu makadinali wanaoweza kumrithi Papa Francis

Wakati huu Vatican ikiwa imeanza maandalizi ya mazishi ya aliyekuwa kiongozi wake Papa Francis ambaye atazikwa wikendi hii, tayari mjadala umeanza kuhusu makadinali wanaoweza kumrithi.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2

Matangazo ya kibiashara

Wa kwanza ni Kadinali Peter Erdo, miaka 72 ni askofu wa Budapest ambaye kwa zaidi ya mara mbili alichaguliwa kuongoza baraza la maaskofu la Ulaya kati ya mwaka 2005 na 2011, akiungwa mkono wenzake wa Ulaya na wale kutoka Afrika.

Kadinali Peter Erdo
Kadinali Peter Erdo AP – Attila Kovacs

Mwingine ni Reinhard Marx, miaka 71 ni askofu wa dayosisi ya Munich, alichaguliwa kuwa mshauri mwandamizi wa Papa mwaka 2023 kabla ya baadae kuteuliwa kusimamia masuala ya fedha ya Vatican.

Kadinali Reinhard Marx
Kadinali Reinhard Marx AP – Alessandra Tarantino

Kadinali Marc Quellet mwenye umri wa miaka 80 raia wa Canada ni mtu mwingine anayepewa nafasi na kwa miongo kadhaa alikuwa kiongozi la jopo la kuchuja makadinali wanaoteuliwa na papa tangu kipindi cha Papa benedict wa 16.

Kadinali Marc Ouellet
Kadinali Marc Ouellet AP – Alessandra Tarantino

Kadinali Pietro Parolin mwenye umri wa miaka 70 ni muitaliano ambaye amekuwa katibu wa papa tangu mwaka 2014, akitajwa kama mmoja ya watu walio vinara kupewa nafasi hiyo.

Kadinali Pietro Parolin akiwa karibu na jeneza la Papa
Kadinali Pietro Parolin akiwa karibu na jeneza la Papa AP – Vatican Media

Kadinali Robert Sarah wa Guinea, ni mtu mwingine anayepewa nafasi ingawa hakuwa na uhusiano mzuri na Papa kutokana na kuwa na msimamo mkali kuhusu tamaduni za kanisa tofauti na papa francis alivyokuwa.

Kadinali Luis Tagle wa Ufilipino, yeye ana umri wa mliaka 67 na huenda akawa Papa wa kwanza kutoka ukanda wa Asia ikiwa atachaguliwa, na aliteuliwa na Papa kuongoza kitengo cha uinjilisti cha Vatican.

Kadinali Robert Sarah
Kadinali Robert Sarah AP – Andrew Medichini

Wemo pia kadinali Matteo Zuppi wa Bolongya mwenye umri wa miaka 69, Robert Prevost raia wa Marekani mwenye miaka 69, kadinali Christoph Schoenborn raia wa Austria mwenye umri wa miaka 80.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *