Weholite na ujenzi wa kesho mpya ya mifumo bora ya usimamizi wa maji

Kuendesha na kudumisha mifu­mo ya usimamizi wa maji sala­ma hakuwezi kufanikiwa bila uwekezaji mpya na utaalamu wa kiufundi, hususan ukizingatia ongezeko la idadi ya watu katika maeneo ya mijini nchini Tanzania.

Matumizi ya mifumo ya mabomba kama vile ya Weholi­te HDPE yanatoa masuluhisho ya muda mrefu dhidi ya changamoto ya usimamizi wa maji ya mvua kubwa ambayo yanaonekana kuharibu maeneo mengi ya mijini, maeneo ya makazi yasiyopang­wa vizuri na mtandao mpana wa uchukuzi nchini kote.

Mifumo ya mabomba makub­wa ya Weholite HDPE yanayo­tengenezwa na Kampuni ya Megapipes Solutions Limited, katika kiwanda chao cha kisa­sa kilichopo Kigamboni, Dar es Salaam, kinatoa njia mbadala na endelevu za kutatua changamoto za mafuriko, maji taka (majum­bani na viwandani) na uhifadhi wa maji nchini Tanzania, kulinga­na na wahandisi wanaotekeleza miradi ya miundombinu.

Mabomba ya DN1800 HDPE Weholite yenye uwazi kwa juu yaliyowekwa katika Mtaa wa Chato, Dar es Salaam.

Miundombinu ya Usafiri

Mitandao ya barabara na reli ya Tanzania inaendelea kupanuliwa kwa kasi, ikichangiwa na ukuaji wa uchumi na hitaji la mifumo bora ya usafiri, na hilo linafan­ya mabomba ya Weholite kuwa bora kwa ujenzi wa barabara kwa sababu yanastahimili kutu na mik­waruzo, ni rahisi pia kufungwa na yanadumu kwa zaidi ya miaka 100.

TANROADS na TARURA zin­aendelea kuwa taasisi za kwanza kutumia teknolojia hii, kwa saba­bu uimara wa asili wa makalvati ya Weholite yameongeza ufanisi na hayana changamoto nyingi. Ujenzi wa barabara sio kwa aji­li ya kupitisha vyombo vya moto pekee, bali unaleta ahueni kubwa kwa jamii kwa ujumla.

Mfano mzuri wa hivi karibuni ni katika kijiji cha Somanga, mkoani Lindi, ambapo barabara kuu muhimu inayounganisha Dar es Salaam, Lindi, na Mtwara ili­athiriwa vibaya wakati mafuriko ya El Niño yaliyolisomba daraja mwezi Mei 2024. Daraja hili lili­kuwa kiungo muhimu cha magari madogo na makubwa yaliyokuwa yakisafirisha mizigo barabarani, hivyo kurahisisha biashara na usa­firishaji katika mkoa huo.

Kadhia hiyo ilileta athari kubwa za kiuchumi, ikizuia na kuchelewesha usafirishaji wa bidhaa kwa ajili ya biashara za ndani. Hata hivyo, kwa kurejelea ufungaji wa makalvati ya Weholi­te uliopita, TANROADS ilichagua kutumia makalvati ya Weholite yenye kipenyo cha DN2000 kujen­ga upya daraja hilo.

Uamuzi huu ulihakikisha kuwa daraja hilo linajengwa upya kwa haraka na ndani ya muda, na kupunguza usumbufu kwa jamii na kuruhusu shughuli za kiuchumi kuendelea kama kawaida.

Miun­do iliyofukiwa chini ya uso wa barabara inahitaji kuwa na sifa za kipekee ili kuhimili mashini­kizo ya kila wakati yanayotoka­na na msongamano mkubwa wa magari unaopita kwenye barabara iliyo juu. Mabomba ya Weholite yameundwa mahsusi kwa kuzin­gatia hili.

Makalvati hayahitaji kuzun­gushiwa zege, badala yake udongo unaofaa kwa ajili ya barabara una mwagwa kila upande wa bomba la Weholite na kushindiliwa. Kuta za pembeni (wing walls) na kuta za juu (head walls) hujengwa ili kuhakikisha udongo haumomon­yoki, jambo ambalo litasaidia pia kuhakikisha kuwa barabara hai­haribiki kunapotokea mafuriko.

Makalvati ya Weholite yan­ayodumu na yenye ufanisi katika kuhakikisha maji yanapitishwa ipasavyo ili yatiririke bila kukatiz­wa. Pia, ujenzi wa mihimili mepesi ya makalvati ya Weholite unara­hisisha uwekaji wake, kuwezesha mtiririko wa maji bila kikwazo, na ni rafiki wa mazingira. Makalva­ti husafirishwa kwa urahisi bila kukatika tofauti na yale ya zege, huu ndiyo mustakabali wa ujenzi wa barabara.

Mifereji ya maji

Ukitembelea barabara za baadhi ya maeneo yenye watu wengi katika miji ya Tanzania zina kitu kimoja cha kufanana, ambacho ni mifereji ya maji iliyo wazi. Hii hupatikana zaidi kati­ka maeneo ya mijini na hutumi­wa kwa kumwaga maji ya mvua, hususan wakati wa mvua kubwa. Maji ya mvua yanayokusanywa na njia hizi mara nyingi huelekezwa kwenye mito au njia nyingine za maji.

Ujenzi wa mifumo ya mifereji ya maji wazi ni utamaduni ambao umedumishwa kwa miongo kad­haa. Dar es Salaam inakabiliwa na mafuriko, na pia ni sehemu ambayo inajulikana sana kwa mifumo ya mifereji ya maji iliy­oziba.

Hali mbaya ya mitaa mingi kwa mfano, inatokana na ujenzi wa mifumo ya mifereji ya maji wazi. Mifereji ya maji inakusudi­wa kusaidia kuzuia mafuriko, hata hivyo, inapoachwa wazi, taka ngu­mu zinaweza kujikusanya ndani yake na kusababisha kuziba na kisha kuleta mafuriko ambayo nayo huharibu barabara.

Kiwango cha uchakavu wa barabara huongezeka kutoka­na na ongezeko la unyevu wa punjepunje na inaonekana wazi kwamba mifereji ya maji iliyo wazi hutumia udongo, ikimaani­sha kwamba hakuna lami au njia za watembea kwa miguu, na hivyo mara nyingi punje hizo hukim­bilia barabarani na kuwa katika hatari ya kukanyagwa na waende­sha magari. Hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari kuokoa mai­sha na mabilioni ya shilingi yan­ayotumika kutokana na magonjwa na uharibifu unaosababishwa na mifereji ya maji wazi.

Kubuni na kutengeneza mifu­mo ya mifereji ya maji kunahitaji ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wahandisi ili kuhakikisha kuwa maji yanatiririka kwa ufanisi na kwa usalama na yanaelekezwa kwenye mkondo wa maji au njia ya maji. Mifereji ya maji iliyowe­kwa na jamii moja haipaswi kule­ta matatizo kwa jamii nyingine chini ya katika mkondo mmoja, wala haipaswi kuathiri maeneo muhimu ya kiikolojia.

Masuluhisho ya Weholite Stormwater (attenuation tanks & pipes systems) yanatoa njia mbadala endelevu za kutatua changamoto za mafuriko jijini Dar es Salaam, kulingana na wah­andisi wanaotekeleza miradi ya miundombinu ya usimamizi wa maji jijini. Weholite hupatikana katika kipenyo cha kati ya DN/ID 350mm hadi DN/ID 3000mm, ambayo yanayafanya kuwa bora kwa kupitishia maji mengi mba­li na maeneo yenye matatizo, na hivyo kuwalinda wakazi dhidi ya kadhia ya mafuriko.

Kampuni ya Megapipes hivi karibuni ilisambaza takribani 300m za DN1800 za mabomba ya Weholite, kwa ajili ya mradi mkubwa wa kukabili mafuriko katika Barabara ya Chato, Dar es Salaam. Mfumo huo ulijumuisha makutano ya barabara kukidhi hitaji maalumu la eneo husika na mashimo kwa ajili ya ukaraba­ti/matengenezo, ambayo hutoa suluhisho la muda mrefu dhidi ya tishio la mafuriko mijini.

Usimamizi wa mifumo ya kud­hibiti maji ya mvua kubwa kati­ka jiji kubwa si kazi nyepesi wala si kitu kisichowezekana kabi­sa unapokuwa na masuluhisho ya Weholite ambayo yanatatua baadhi ya changamoto zetu za uhandisi.

Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na kuweka miundombinu kwa njia ambayo inahatarisha maisha ya wakazi milioni sita wa jiji la Dar es Salaam. Mabomba ya Weholite ni mepesi zaidi kuliko mifumo ile ya zege ambayo hura­hisisha usafirishaji na usimamizi wake kuwa sio tu wa haraka lakini nafuu na salama.

Weholite ndiyo bidhaa inayo­faa zaidi kwa mifumo ya mifereji ya maji ya mvua kama ile iliyo­fungwa katika Barabara ya Chato, kutokana na utengamano wake na uwezo wa kubuniwa kwa urahisi katika mipangilio tofauti, ambayo vinginevyo ingekuwa vigumu sana kujenga kwa kutumia mbinu zilizozoeleka. Hii ni sifa muhimu inayohotajika wakati mfumo unapolazimika kukabiliana na changamoto za maeneo ya mijini yenye watu wengi na wingi wa huduma nyingine ambazo ziko chini ya ardhi.

Faida nyingine ni kwamba Kam­puni ya Megapipes iliweza kuun­ganisha na kufanya majaribio ya sehemu zilizojengwa kwenye kiwanda chao Kigamboni, Dar es Salaam na kupunguza muda wa ufungaji miundombinu kwenye eneo la mradi na kuongeza imani kwa mteja. Kwa kuongezea, taka ngumu zinashughulikiwa kwa usalama kupitia hydraulics bora za mifereji ya maji taka iliyofung­wa tofauti na ile iliyo wazi.

Mradi wa Barabara ya Cha­to unaotekelezwa na TARURA Kinondoni unatarajiwa kuboresha maisha ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambao wanakabiliwa na mafuriko kila mara. Hivi sasa, mafuriko yanaathiri moja kwa moja na kwa njia isiyo ya moja kwa moja wakazi wawili kati ya watano wa jiji hilo au karibu watu milioni mbili kwa viwango tofauti.

Suluhisho hili jipya na bunifu linaleta thamani kubwa kwa waka­zi wa Dar es Salaam, kwa kuwa ni teknolojia iliyotengenezwa nchini na kuthibitishwa, ambayo imeku­wa ikitumika duniani kote kuanzia Afrika Kusini, Ulaya na Amerika Kaskazini.

Mustakabali wa usimamizi wa maji

Mabomba na mifumo ya Weho­lite HDPE inaweza kubuniwa kukidhi ya mtu mmoja mmoja au taasisi katika mazingira yaliyo­jengwa, au vivyo hivyo kutumi­ka kwenye ujenzi wa haraka wa miundombinu ya usafiri kwenye barabara kuu, barabara za miji­ni au mazingira ya vijijini; hivyo, kuwaondolea wahandisi chan­gamoto iliyopo ya uwekaji miun­dombinu nchini.

Kadhia zinazoletwa katika maisha ni mojawapo ya sababu kuu ambazo jamii mara nyingi hupinga utekelezwaji wa miradi mipya, jambo ambalo halipatikani unapotumia bidhaa za Weholite. Yote inamaanisha kwamba tekno­lojia hii inapaswa kutumiwa kwa uwezo wake wa kufunga miun­dombinu hii mpya kwa njia ya haraka na ya ufanisi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *