JKT Queens yaendeleza rekodi za vipigo WPL

ACHANA na msimamo ulivyo wa Ligi ya Wanawake, JKT Queens ikiwa kileleni na pointi 38, timu hiyo inaongoza kwa kutoa vichapo kama ilivyo kauli mbiu yao ‘Kichapo cha Kizalendo’.

Msimu huu imetoa vipigo vitanpo hadi sasa sawa na ilivyotoa msimu uliopita wote na tayari imefunga mabao 56 ikiwa timu pekee iliyofunga mabao kuanzia 50 kwenye mechi 14, huku Simba ikiweka kambani 46 tofauti ya mabao 10.

Msimu huu timu hiyo ikiwa kwenye mbio za ubingwa imezifunga baadhi ya timu mabao kuanzia mabao matano na kuendelea kama ilivyokuwa msimu wa kwanza ulipochukua ubingwa.

12-0 Mlandizi Queens Februari 04

5-0  Mashujaa Queens Machi 19

5-0  Ceasiaa Queens Machi 23

7-0  Mlandizi Queens

6-0  Ceasiaa Queens

Hii sio mara ya kwanza kwa timu hiyo kutoa vichapo hivyo, kwani ishafanya hivyo msimu uliopita ilipomaliza ligi ikifunga mabao 54 na kuruhusu saba.

Kiufupi msimu huu zikiwa zimesalia mechi nne, tayari timu hiyo imevunja rekodi ya msimu uliopita na safu ya ushambuliaji msimu huu inaonekana kuwa bora zaidi ikifunga mabao hayo huku ikisubiriwa kama itatoa kichapo kingine kikubwa na kuipita rekodi ya msimu uliopita.

Msimu 2017/18, ndiyo mwaka ambao JKT ilinyakua ubingwa wa WPL kwa mara ya kwanza ilipotoa vipigo vya mabao matano au zaidi kwa baadhi ya timu ikiwamo Simba Queens.

Novemba 26, 2017

JKT Queens 9-0 Mlandizi Queens

Asha Mwalala (manne)

Fatuma Mustafa (mawili)

Stumai Abdallah

Donisia Minja

Anna Katunzi

Novemba 29, 2017

JKT Queens 9-0 Fair Play

Hat-trick kila mmoja

Asha Mwalala

Stumai Abdallah

Fatuma Mustafa

Desemba 3, 2017

JKT Queens 5-0 Evergreen Queens

Donisia Minja

Asha Mwalala (mawili)

Fatuma Mustafa

Stumai Abdallah

Desemba 6, 2017

JKT Queens 5-1 Mburahati Queens

Fatuma Mustafa (mawili)

Stumai Abdallah (hat-trick)

Desemba 9, 2017

JKT Queens 5-2 Simba Queens

Asha Mwalala (mawili)

Stumai Abdallah

Fatuma Mustafa

Fatuma Mwisendi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *