Ethiopia yaahidi kutumia fursa za biashara huria kutoa fursa zaidi barani Afrika

Waziri wa Biashara na Ushirikiano wa Kikanda wa Ethiopia amesema kuwa, nchi yake ina nia thabiti ya kuhakikisha kunakuwepo utekelezaji madhubuti wa makubaliano ya Eneo Huria la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA) ili kutoa fursa kubwa za soko la ndani ya bara pana na kubwa la hilo.